Nafasi Ya Matangazo

June 30, 2017



 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo , Nuru Millao (kushoto) na Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini , Roeland Van De Geer (kulia) wakifunua kitambaa kuonyesha jiwe la msingi linaashiriwa kufunguliwa kwa  Kituo  cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii kilichopo katika jengo la Old Boma leo Jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Nuru Millao akitoa hotuba kwa niaba ya Waziri wa Wizara hiyo Mhe.Dkt. Harrison Mwakyembe katika hafla ya kufungua kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo  na Utalii kilichopo katika jengo la Old Boma leo Jijini Dar es Salaam.




Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita akiongea na wageni (hawapo katika picha) wakati wa hafla ya kufungua  Kituo  cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii  kilichopo katika jengo la Old Boma leo  Jijini Dare s Salaam.



 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bibi. Nuru Millao (mwenye mtandio) akiwa katika picha na wageni waliohudhuria hafla ya ya kufungua kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo kilichopo katika jengo la Old Boma na Utalii leo Jijini Dar es Salaam.


NAIBU Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo , Nuru Millao  ameupongeza Uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kulifanya jengo la Old Boma kuwa Kituo cha Urithi wa Ubunifu wa Majengo na Utalii (DARCHI).Anaandika Lorietha Laurence- WHUSM.



Akizungumza katika hafla ya kufungua  kituo  hicho leo Jijini Dar es Salaam kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt.Harrison Mwakyembe, Millao alisema hatua hiyo inadhihirisha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha kuwa utamaduni wa Mtanzania unadumishwa na kukuzwa.

“Ni dhahiri kuwa wananchi  wataweza kufahamu umuhimu wa kutunza na kuhifadhi majengo ya kale kutokana na elimu watakayoipata kupitia kituo hiki katika kukuza utamaduni ” alisema Millao.

Aidha alitoa wito kwa kwa Jumuiya ya Wasanifu Majengo Tanzania kuendelea kushirikiana na Taasisi za ndani na nje ya nchi katika kutekeleza mipango ya kutunza majengo na sehemu za kale ili  kuhifadhi historia na utamaduni wa Mtanzania.

Pia amezitaka Mamlaka za Serikali za Mitaa katika Jiji la Dar es Salaam kusimamia sheria kwa  kushughulia kero mbalimbali zinazotokana na udhaifu wa sheria za kuendeleza majengo ya kale.

Naye  Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita ameeleza kuwa kufunguliwa kwa  kituo hiko ni fursa ya kukuza pato la uchumi wa nchi kupitia mapato ya watalii watakaokitembelea.

 “Tayari tumeweka mipango mbalimbali ya kuhakikisha Jiji letu la Dar es Salaam linakuwa sehemu ya Utalii kwa kutoa mafunzo kwa madereva Taxii ambao wanahusika katika kuwasafirisha  watalii ili wawe na uelewa zaidi kuhusu kituo hiki ” alisema Mstahiki Meya Mwita.

Kwa Upande wake Balozi wa Umoja wa Ulaya Nchini, Roeland Van De Geer amesema ofisi yake iko tayari kushirikiana kwa karibu na Jiji la Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla katika kuleta maendeleo.
Posted by MROKI On Friday, June 30, 2017 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo