Nafasi Ya Matangazo

March 01, 2017

Na Bety Alex, Arusha
JESHI la polisi kwa mkoa wa arusha limefanikiwa kukamata bunduki 10 pamoja na risasi 59  ambazo zilikuwa zinatumika kwenye matukio mbalimbali ya uhalifu

Risasi 59 ambazo zilikuwa zinatumika na wananchi wa maeneo ya Ngorongoro mkoani Arusha na taarifa za awali zinaonesha kuwa zilikuwa zinatumika kwenye ujangili.

Akiongea na vyombo vya habari mapema leo kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Charlz Mkumbo alisema kuwa kunaswa kwa silaha hizo kunatokana na oparesheni iliyofanyika kwa zaidi ya wiki mbili nakuhusisha maeneo mbalimbali mkoani Arusha.

Mkumbo amesema kuwa katika kijiji chaMagaiduru Kata ya Olorien  Tarafa ya Loliondo silaha aina ya Chinese 56 smg yenye namba MT .70 B 1 2730021 ikiwa na magazine yenye risasi 21 ilikutwa  katika ofisi ya kijiji baada ya kutelekezwa na mtu asiyejulikana . 
 
Ameongeza kuwa katika kijiji cha Oldonyosambu ilipatikana silaha aina ya mark 1V  yenye namba ZKK 5602 iliyotelekezwa kwenye kichaka ambapo katika kijiji cha jema kata ya oldonyosambu askari waliokuwa katika operesheni hiyo walifanikiwa kupata silaha nne aina ya Chinese 56 smg pamoja na risasi 19.

Katika hatua nyingine  kamanda amedai kuwa muwemdelezo wa operesheni hiyo ulizidi kufanikisha kupata silaha tatu katika kijiji cha Sale Tarafa ya Sale ambazo ni Chinese 56 SMG yenye namba 89020539 ikiwa na risasi 15 pamoja na S.A.R yenye namba 263126  zilipatikana na hivyo kusababisha operesheni hiyo kukamata jumla ya silaha kumi za aina nne tofauti pamoja na risasi 59.

Hataivyo  jeshi hilo mkoani hapa limetoa onyo kali kwa wakazi wote wa arusha wanaomiliki silaha kinyume cha sheria wazisalimishe mara moja katika ofisi za mtaa au kijiji kwani watakuwa katika mkono salama na atakayekaidi amri hii hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.
Posted by MROKI On Wednesday, March 01, 2017 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo