Nafasi Ya Matangazo

November 09, 2016

Na Bety Alex, FK Blog-Arusha
Katika hali isiyokuwa ya kawaida Mkuu wa Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha,  Alexander Mnyeti,      ameagiza wenyeviti wa vijiji katika Wilaya hiyo kuwapa adhabu kali baadhi ya wazazi na walezi ambao watabainika kuingia kwenye majumbaa ya starehe na pombe wakiwa wameambatana na watoto wao.

Hataivyo adhabu hizo ni pamoja na kuwatandika viboko hadharani wazazi hao kwa kuwa hawawajengi watoto vema

Aliyasema hayo wiki iloyopita wakati akiongea na wenyeviti wa vijiji kutoka katika vijiji vyote vya wilaya hizo.

Aidha mnyeti alifafanua kuwa haipendezi hata kidogo kwa baadhi ya wazazi kujisahau suala zima la malezi hadi wafikie hatua ya kutaka kwenda kwenye majumba ya starehe na watoto

Aliongeza hiyo ni tabia ya kupingwa na kukataliwa kabisa na wadau pamoja na uongozi wa kata na endapo watakapombaini muhusika basi wanatakiwa kumpa adhabu Kali.

"Nimewapa mamlaka kabisa ya kuwachapa viboko ambao watabainika kufanya hivi na mkifanya hivi itawajengea jamii tabia nzuri'aliongeza Mnyeti.

Wakati huo huo aliwataka wenyeviti pamoja na watendaji pia kuwapa adhabi kali baadhi ya vijana ambao watajihusisha na unywaji wa pombe za kawaida na haramu wakati wa kazi.

Alibainisha kuwa unywaji wa pombe wakati wa kazi sio tendo zuri hata kidogo na kwa hali hiyo pia mnatakiwa kutoa adhabu kali kwa wote watakaokutwa 'Hakikisheni kuwa mnawatandika ipasavyo wote ambao watakutwa na kosa hili kwani ninyi mna uwezo mkubwa wa kutengeneza hii jamii'aliongeza Mnyeti

Akiongea kwa niaba ya wenyeviti mmoja wa wenyeviti hao,Luca Daniel alisema kuwa wananchi wanapaswa kutii mamlaka ambazo zipo na kama watafanya hivyo wataweza kuruhusu amani kuwa ya kudumu.
Posted by MROKI On Wednesday, November 09, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo