Nafasi Ya Matangazo

November 07, 2016



Naibu Waziri wa Fedha na Mipango ambaye pia ni Mbunge wa Kondoa Vijijini, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akipokea madawati 100 yenye thamani ya Milioni 10 kutoka kwa Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TPB, Jema Msuya. Makabidhiano hayo yalifanyika wilayani Kondoa, Dodoma



Naibu Waziri wa Fedha na Mipango ambaye pia ni Mbunge wa Kondoa Vijijini, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akipokea madawati 100 yenye thamani ya Milioni 10 kutoka kwa Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TPB, Jema Msuya. Makabidhiano hayo yalifanyika wilayani Kondoa, Dodoma



Naibu Waziri wa Fedha na Mipango ambaye pia ni Mbunge wa Kondoa Vijijini, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akiwa katika picha ya pamoja na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TPB, Jema Msuya baada ya Makabidhiano ya Madawati 100 yenye thamani ya shilingi milioni 10, Makabidhiano hayo yalifanyika wilayani Kondoa, Dodoma. Wa kwanza kulia Meneja wa TPB tawi la Dodoma, Twaha Khaflani, wengine ni viongozi wa Wilaya ya Kondoa.

Benki ya Posta Tanzania (TPB) imetoa msaada wa madawati 100 yenye thamani ya zaidi ya milioni 10 kwa ajili ya shule za msingi za Wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma. Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo Kaimu Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania, Jema Msuya alisema wametoa msaada huo ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya tano kwenye sekta ya elimu.

Msuya alisema misaada inayotolewa na benki hiyo ni sehemu ya gawio la faida inayopata benki na kuirudishia jamii kwa kuwajengea au kuunga mkono miradi ya maendeleo. Alisema misaada hiyo inatokana na maombi ya misaada ya iliyotumwa kwao na Viongozi au Wananchi kwa miradi ya maendeleo lakini benki imekuwa ikitoa kulingana na bajeti yake inavyoruhusu. 

Hata hivyo alisema mpaka sasa benki hiyo imeshatoa madawati zaidi ya 300 mwaka huu na kujenga vyoo na vyumba vya madarasa katika Mikoa mbalimbali hapa Nchini. Aidha aliongeza kuwa TPB imekuwa ikiunga mkono Serikali kwa kusaidia Jamii katika sekta ya afya, elimu na ustawi wa jamii.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa fedha na Mipango ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Kondoa Vijijini, Dkt. Ashatu Kijaji aliishukuru TPB kwa kutoa msaada huo. Dkt. Kijaji alisema Serikali inatakiwa kuungwa mkono na wadau wa maendeleo ili kuweza kufanikiwa katika malengo iliyojiwekea ya kuwahudumia Wananchi. “kwa upendeleo wa kipekee naomba  katika madawati  haya 100 tuliyopewa madawati 50 yaende shule msingi Kalamba  niliyosoma mimi” aliomba Naibu Waziri.

Naye Afisa Elimu Wilaya Kondoa, Alphonce Mwamwile alisema Wilaya hiyo ina upungufu wa madawati 5765 yanayohitajika. Aidha aliwaomba wadau wengine kujitokeza kusaidia changamoto ya madawati na vyumba vya madarasa katika Wilaya ya hiyo ili Wanafunzi waweze kusoma na kuandika vizuri wakiwa darasani.
Posted by MROKI On Monday, November 07, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo