Nafasi Ya Matangazo

November 18, 2016

 Afisa Mradi, Kitengo cha Kujenga Uwezo kutoka shirika lisilo la Kiserikali la  ‘The Foundation For Civil Society’ Nasim Losai, akitoa mada wakati wa ufungaji wa Tamasha la Tano la Watu wenye Ulemavu lililoanza jana Nov 16, 2016 kwenye Hoteli ya Blue Pearl Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam. Tamasha hilo limefungwa hii leo hayo. 
 Mkufunzi Mwelekezi, Salma Maoulid, akisimamia zoezi la maswali na majibu wakati wa kufunga Tamasha la Tano la Watu wenye Ulemavu lililoanza jana kwenye Hoteli ya Blue Pearl Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam.
 Afisa Uchumi Mwandamizi, Mchambuzi na Mipango, Andrea Aloyce, akitoa mada kwa washiriki wakati wa kufunga Tamasha la Tano la Watu wenye Ulemabu lililoanza jana Nov 16, 2016 kwenye Hoteli ya Blue Pearl – Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam.
 Mshereheshaji akiendelea kuongoza Tamasha hilo
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Governance & Economic Policy Centre, Moses Kulaba, akitoa mada kwa washiriki wakati wa kufunga Tamasha la Tano la Watu wenye Ulemabu lililoanza jana Nov 16, 2016 kwenye Hoteli ya Blue Pearl – Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam. 
 Mkarimani akiwatafsiria walemavu Viziwi kila kilichokuwa kikizungumzwa ukumbini hapo
 Mshereheshaji akiendelea kuwachangamsha washiriki, ''Abunuasi aliwauliza Je mnajua lichowaitia?? wakajibu hapana, akwaambia basi kama hamjui basi rudini nyumbani, wakaru, Siku yapili Je mnajua nilichowaitia?? wakajibu Ndiyooo,akawaambi basi kama mnajua basi rudini nyumbani kwa sababu mnajua ninachotaka kuzungumza nanyi, ikabidi waondoke, Siku ya Tatu wakaja tena alipo wauliza Je mnajua nilichowaitia??? siku hiyo wakakubaliana kujigawa wengine wakasema Ndiyoooo, na wengine wakajibu Hapanaaaa, akawaambia basi sasa itabidi nyie mnaojua muwaambie hao wasiojua kile ninachotaka kuzungumza, kisha mrudi nyumbani'' kila mmoja akaguna na kuondoka mahala hapo kwa hasira....
 Mshiriki akiongozwa kuingia ukumbini.
 Waratibu wa Tamasha hilo wakiwa bize kuratibu yaliyokuwa yakiendelea ukumbini hapo wakati wa kufunga Tamasha hilo. 
 Mshiriki akiuliza swali.
 Sehemu ya washiriki wa Tamasha hilo wakifuatilia kilichokuwa kikiendelea ukumbini hapo.
Posted by MROKI On Friday, November 18, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo