Nafasi Ya Matangazo

November 04, 2016



Rais John Magufuli akijibu maswali kutoka kwa waandishi wa habari na wahariri wakati wa mkutano wake wa kwanza kufanya mahojiano na waanahabari tangu aingie madarakani Novemba 5,2015. Mahojiano haypo maalum na ya aina yake yalifanyika Ikulu jijini Dar es Salaam leo.
Rais John Magufuli akijibu maswali kutoka kwa waandishi wa habari na wahariri wakati wa mkutano wake wa kwanza kufanya mahojiano na waanahabari tangu aingie madarakani Novemba 5,2015. Mahojiano haypo maalum na ya aina yake yalifanyika Ikulu jijini Dar es Salaam leo.
 Wahariri wa vyombo vya habari wakifuatilia kwa makini mahojiano hayo.
 Bloggers ni miongoni mwa wanahabari waliopata fursa hiyo ya kushiriki katika mkutano huo.
Rais Dk John Pombe Magufuli leo Novemba 4, 2016 kwa mara ya kwanza tangu aingie madarakani mwaka mmoja uliopita, amefanya mahojiano na Wahariri na Waandishi wa Habari wa vyombo mbalimbali vya habari vya ndani na nje ya nchi katika ukumbi wa Ikulu jijini Dar es Salaam.

Mahojiano hayo yaliyorushwa moja kwa moja (Live) kupitia vyombo vya habari vya Redio, Televisheni na Mitandao yamechukua muda wa saa 2 na dakika 40 ambapo Rais Magufuli ametumia nafasi hiyo kujibu maswali yote yaliyoulizwa na wahariri na waandishi wa habari na ambayo yalilenga kujua utendaji kazi wa Serikali ya awamu ya tano katika kipindi cha mwaka mmoja tangu iingie madarakani.

Katika majibu yake Rais Magufuli amesema katika kipindi cha mwaka mmoja Serikali yake imehakikisha nchi inaendelea kuwa na amani, utulivu na umoja na pia imechukua hatua madhubuti za kuchochea kasi ya maendeleo zikiwemo kuongeza ukusanyaji wa mapato kutoka Shilingi Bilioni 800 hadi kufikia wastani wa Shilingi Trilioni 1.2, Kununua ndege kwa ajili ya kurahisisha usafiri na kukuza sekta ya utalii, kuongeza bajeti ya maendeleo katika bajeti ya Serikali kutoka asilimia 26 hadi kufikia asilimia 40 na kujenga miundombinu ya barabara na madaraja.

Dkt. Magufuli amezielezea hatua nyingine kuwa ni kulipa madeni ya ndani na nje ya nchi, kuongeza mikopo ya wanafunzi wa vyuo vikuu, kuongeza fedha za kununulia dawa na chanjo, kubana matumizi kwa kuelekeza fedha nyingi katika utatuzi wa kero za wananchi na kuimarisha uhusiano na ushirikiana na nchi mbalimbali duniani kwa lengo la kuvutia uwekezaji katika viwanda, utalii, miundombinu na huduma za kijamii.

Aidha, ameongeza kuwa Serikali imeweza kutoa fedha za ruzuku kwa shule za msingi na sekondari kiasi cha shilingi Bilioni 18.77 kila Mwezi kwa ajili ya kuwezesha utoaji wa elimu bila malipo, imetoa fedha kiasi cha Shilingi Bilioni 148 kwa ajili ya upanuzi wa mradi wa kuzalisha umeme wa Kinyerezi I na uanzishaji wa mradi wa umeme wa Kinyerezi II.

Kufuatia hatua hizo na nyingine nyingi, Rais Magufuli amesema katika mwaka mmoja wa uongozi wake nchi imeshuhudia ukuaji mzuri wa uchumi wa wastani wa asilimia 7.9 katika robo ya pili ikilinganishwa na asilimia 7 ya mwaka jana na kupunguza mfumuko wa bei kutoka zaidi ya asilimia 7 hadi kufikia asilimia 4.5 hivi sasa.

Dkt. Magufuli amesema amedhamiria kuhakikisha Serikali inarekebisha kasoro zilizokuwa zikisababisha upotevu wa mali ya umma, vitendo vya ulaji rushwa na uhujumu uchumi, matumizi mabaya ya madaraka na kuijenga Tanzania mpya ambayo kila Mtanzania atanufaika na rasilimali za nchi yake.

Rais Magufuli ametoa wito kwa vyombo vya habari kufanya kazi zake kwa kutanguliza uzalendo, kuepuka kutumiwa na watu wenye nia ya kutetea maslai yao binafsi, kuepuka kuchochea vurugu na uvunjifu wa amani na kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali kurekebisha kasoro zilizokuwa zikisababisha nchi kwenda vibaya.

Dkt. Magufuli amewapongeza Wahariri na Waandishi wa Habari kwa kazi kubwa wanayoifanya na amewaahidi kuwa Serikali yake itaendelea kushirikiana nao ili kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi kuhusu utendaji kazi wa Serikali na maendeleo ya nchi yao.
Posted by MROKI On Friday, November 04, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo