Nafasi Ya Matangazo

November 28, 2016

Father Kidevu Blog , Arusha
MBUNGE Godbless Lema wa Arusha mjini leo ameshindwa kupata dhamana ya kutoka rumande baada ya mawakili wa serikali kutoa pingamizi la rufaa.

Mawakili wa serikali wakiongozwa na Martenus Marandu  waliwaambia waandishi wa habari kuwa waliweka pingamizi kuwa upande wa mshtakiwa  walipaswa kupeleka notisi ya kusudio ya kukata rufaa na sio kukata rufaa kama walivyofanya.

Akizungumza nje ya Mahakama hiyo wakili wa upande wa mhishatakiwa Peter Kibatala alisema kesi hiyo itasikilizwa kwa njia ya majibishano ya barua Novemba 30 ambapo upande wa serikali  utatakiwa kuwasilisha hoja zao majira ya sa mbili asubui, huku upande wa mhishatakiwa lema ukitakiwa kuwasilisha majibu ya hoja hiyo majira ya saa sita mchana na upande wa serikali watapaswa kujibu hoja ya upande wa mshitakiwa majira ya saa tisa alasiri.

Mahakama hiyo inatarajia kutoa  uamuzi juu ya pingamizi hilo Desemba 2, majira ya saa tatu asubuhi  huku mshitakiwa akirudishwa rumande hadi tarehe hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mahakamani hapo mwenyekiti wa Chadema   mkoa  wa Arusha, Amani Golugwa kimelaaani hatua hiyo na kuitaka Mahakama itende haki juu ya shauri la Mbunge huyo kwani wanashindwa kuelewa ni kitu gani kinachofichwa katika mwenendo wa shauri hilo.
Posted by MROKI On Monday, November 28, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo