Nafasi Ya Matangazo

August 17, 2016


 Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Adam Mayingu, akifunga mafunzo hayo Agosti 16, 2016
 Meneja wa PSPF, anayeshughulikia Mpango wa Uchangiaji wa Hiari, (PSS), Mwanjaa Sembe, akitoa mada kuhusu faida za kujiunga na mpango huo
 Kaimu Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, (NHIF), Mkoa wa Ilala, Hipoliti Lello, akitoa mada kuhusu huduma zitolewazo na Mfuko huo hususan ushirikiano wa Mfuko huo na PSPF, katoa bima ya afya kwa wanachama wa PSPF
 Mkuu wa Wilaya Mstaafu, Betty Mkwasa, akifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zikitolewa kwenye mafunzo hayo
  Mkuu wa Wilaya Mstaafu, Manzie Manguchie, akifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zikitolewa kwenye mafunzo hayo
 Mwenyekiti wa Wakuu wa Wilaya Wastaafu, Ramadhan Maneno, (kushoto), akizungumza jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Global Publisher, Eric Shigongo
 Mkuu wa Wilaya Mstaafu, Makunga, akitoa maoni yake kuhusu uanzishwaji wa SACCOS hiyo. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.
NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
WAKUU wa wilaya wastaafu, wameunda Ushirika wa Kuweka na Kukopa, (SACCOS), ikiwa ni moja ya maazimio waliyotoka nay oleo Agosti 16, 2016, baada ya semina ya mafunzo ya siku mbili, iliyolenga kuwaelimisha namna bora ya kuwa wajasiriamali.
Akitangaza azimio hilo, mwishoni mwa mafuno hayo yaliyofadhiliwa na Mfuko wa Pensheni wa PSPF, na kufanyika makao makuu ya Mfuko huo jijini Dar es Salaam, Mjumbe wa Sekretariati ya wakuu hao wastaafu, Crispin Meela, alisema, wajumbe 10 wamechaguliwa na wana semina hao ili kushughulikia utaratibu mzima wa kuanzishwa kwa SACCOS hiyo haraka iwezekanavyo.
Wajumbe wa Kamati ya muda ya kusimamia mambo hayo ni pamoja na Ramadhan Maneno (Mwenyekiti), Betty Mkwasa (Katibu), Crispin Meela, Erasto Sima, Geogina Bundala, Farida Mgomi, Said Amanzi, Fatma Ally, Muhingo Rweyemamu na Manzie Mangochie.
Kwenye mafunzo hayo Wakuu hao wa wilaya wastaafu, waliweza kupata elimu kutoka kwa wataalamu mbalimbali wakiwemo Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Beng’ Issa, na wataalamu wa Saikolojia, na Wajasiriamali wenyewe kama vile Eric Shigongo.
Akifunga mafunzo hayo Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Adam Mayingu, ametoa changamoto kwa wakuu hao wanaokadiriwa kufikia 100 na ambao wamejiunga uanachama wa Mfuko huo kupitia mpango wa uchangiaji wa Hiari, (PSS), kuwa uamuzi wao utawakwamua kiuchumi na wanachotakiwa ni kuwa na mpango kamambe utakaoweza kutekelezeka kwa ufanisi mkubwa.
“PSPF kama shirika lingine lolote lile la kutoa huduma za Pensehni na za kifedha, umoja huo ni fursa kubwa kwa Mfuko na ndio maana umeamua kuwaunga mkono  ili mmfikie azma yenu ya kuanzisha SACCOS hiyo”. Alisema.

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Global Publishers, Eric Shigongo, akitoa mada juu ya ujasiriamali kwa Wakuu wa Wilaya wastaafu, wakati wa semina ya mafunzo ya ujasiriamali yaliyofadhiliwa na Mfuko wa Pensheni wa PSPF, na kufanyika makao makuu ya Mfuko huo jijini Dar es Salaam, Agosti 16, 2016.


 Mwenyekiti wa Wakuu wa wilaya wastaafu, Ramadhan Maneno
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, (TAMISEMI), George Simbachawene, (watatu waliokaa), Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashantu Kijaji, (wapili waliokaa), Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya PSPF, George Yambesi, (wapili kulia), Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Adam Mayingu, (wakwanza kushoto waliokaa) na Mwenyekiti wa Wakuu hao wa Wilaya wastaafu, Ramadhan Maneno, (wakwanza kulia waliokaa) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wastaafu hao
 Mkuu wa Wilaya Mstaafu, Erasto Sima
 Mkuu wa Wilaya mstaafu, Christopher Kangoye
 Shigongo, akisalimiana na Mkuu wa wilaya mstaafu, Mwalimu Zainabu R.M. Mbussi
 Meneja wa PSS, Mwanjaa Sembe, akimsikiliza Mkuu wa wilaya mstaafu, Erasto Sima
 Shigongo akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wakuu wa wilaya wastaafu, baada ya kuwapa elimu juu ya ujasiriamali
 Shigongo akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa PSPF
 Shigongo akisikiliza maswali ya wakuu wa wilaya wastaafu baada ya kutoa mada yake, iliyowavutia wengi
 Kaimu Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, (NHIF), Mkoa wa Ilala, Hipoliti Lello, (kushoto), akizungumza jambo na Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Abdul Njaidi, (kulia) na Mtafiti wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Mapesi Maagi
 Shigongo aiasikiliza wakuu wa wilaya wastaafu baada ya kutoa mada yake juu ya ujasiriamali
 Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Adam Mayingu, (wapili kushoto), akipokewa na Mwenyekiti wa Wakuu wa wilaya wastaafu, Ramadhan Maneno, (watatu kushoto), Katibu wa wakuu hao, Betty Mkwasa, (kushoto) na Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko huo Abdul Njaidi wakati akielekea ukumbini kufunga mafunzo hayo Agosti 16, 2016
 Mgeni rasmi na wakuu hao wa wilaya wastaafu
  Mgeni rasmi na wakuu hao wa wilaya wastaafu
Posted by MROKI On Wednesday, August 17, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo