Nafasi Ya Matangazo

August 23, 2016

NIGERIA NA TANZANIA KUCHEZA SEPTEMBA 3
 Shirikisho la Mpira wa Miguu Nigeria (NFA), limesogeza mbele kwa siku moja mchezo kati ya timu ya taifa ya Nigeria ‘The Super Eagles’ na Tanzania ‘Taifa Stars’ ambako sasa utafanyika Septemba 3, 2016 badala ya Septemba 2, 2016 iliyotangazwa awali.

Na Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa kesho anatarajiwa kutangaza kikosi ambacho atakiandaa maalumu kwa mchezo huo. Mkwasa amesema kwamba anatarajia kuita wachezaji 20 ambao atasafiri nao kwenda Nigeria kwa ajili ya mchezo huo.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hii  BOFYA HAPA


IVORY COAST YAWASILI DAR, MECHI IJUMAA
 Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu Ufukweni ya Ivory Coast, imeingia Dar es Salaam, Tanzania leo saa 8.00 usiku kwa ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia ikitokea jijini Abidjan.

Timu hiyo imekuja Dar es Salaam kwa ajili ya mchezo wa kwanza wa kuwania nafasi ya kucheza Kombe la Mataifa ya Afrika kwa mpira wa miguu wa ufukweni ambako itacheza na wenyeji Tanzania Ijumaa wiki hii kwenye uwanja maalumu ulioandaliwa kwa ajili ya mchezo huo.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hii BOFYA HAPA

TFF YAIANDALIA SERENGETI BOYS KAMBI TULIVU
Baada ya kutekeleza ahadi ya mwanzo ya kuipeleka Madagascar kwa ajili ya kambi ya kuivaa Afrika Kusini ‘Amajimbos’, Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amepanga kutekeleza ahadi yake nyingine kwa kuipeleka timu ya taifa ya Tanzania ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’ kwenye kambi tulivu, ikiwezekana nje ya nchi.

Rais Malinzi aliahidi na kutekeleza ahadi yake kuipeleka Madagascar Serengeti Boys baada ya kuitoa Shelisheli katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazofanyika Madagascar, mwakani. Kadhalika aliahidi kuipeleka timu hiyo nje ya nchi ambayo hata hivyo haijateuliwa baada ya kuindoa Afrika Kusini. Ameahidi kambi hiyo itaanza Septemba mosi, mwaka huu.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hii BOFYA HAPA 
Posted by MROKI On Tuesday, August 23, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo