Nafasi Ya Matangazo

August 23, 2016

Mbunge wa Ileje Mh Janet Mbene, akiwa na watendaji wa Halmashauri hiyo  akikagua sehemu ya juu ya jengo jipya la Hospitali ya Wilaya ya Ileje Ksata ya Itumba inayojengwa kwa pesa za Serikali ya Tanzania
 Mganga mkuu wa Hospitali ya  Ileje akitoa maelezo kwa  Mbunge wa Jimbo hilo Mh Janet Mbene alipokuw akaikagua ujenzi wa jengo jipya la Hospitali hiyo.
 Mbunge wa Ileje Mh Janet Mbene akitoa pole katika wodi ya Wanawake amabao walibahatika kujifungua kwa Upasuaji katika Hospitali ya Wilaya ya Ileje.
 Mbunge wa Ileje Mh Janet Mbene akitoa pole katika wodi ya Wanawake amabao walibahatika kujifungua kwa Upasuaji katika Hospitali ya Wilaya ya Ileje. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.

  Mbunge wa Ileje Mh Janet Mbene akiwa amembeba mmoja ya watoto waliozaliw akatika hospitali ya Wilaya ya Ileje


  Mbunge wa Ileje Mh Janet Mbene akikagua mashine ya X -Ray  katika Hospitali ya Wilaya ya Ileje
  Mbunge wa Ileje Mh Janet Mbene akipita katika moja za wodi za Hospitali ya Wilaya ya Ileje


Na Mwandishiwetu,  Ileje
MBUNGE wa Ileje  Mh Janet Mbene,  amemtaka mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo  kuwachukulia hatua wale wote ambao wamehusika katika ubadhilifu wa fedha za mradi wa ujenzi wa Hospitlai ya Wilaya ya Ileje.

Mh Mbene alisema hayo alipofanya ziara katika Hospitali hiyo na kubaini upungufu mkubwa juu ya muda wa ujenzi wa Hospitali hiyo na kiasi cha pesa kilichotolewa na Wizara ya fedha katika kaukamilisha ujenzi huo ambao kwa sasa umekwama.

"Naomba Mkurugenzi afikishe swala hili kwa TAKUKURU, hili waweze kubaini ni kiasi gani ambacho kimeibiwa na wale wote waliohusika kuchukuliwa hatua kali za kisheria hasa kwa mujibu wa sheria za utumishi wa Umma na kushtakiwa katika Mamlaka zinazo husika" alisema Mbene.

aliweka wazi kuwa inaonyesha wazi kuwa wakati wa kuvunja bara za la madiwani kiasi cha pesa zaidi ya milioni 100 kilikuwepo kwenye akaunti kwa jaili ya ujenzi wa jengo jipya la Hospitali ya Wilaya ya Ileje lakini mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi na kikao cha kwanza cha baraza la Madiwani fedha hizo azionekani zilipokwenda.

anataja kuwa kumekuwa na utamaduni wa watendaji kutumia fedha kinyume na mipango hali inayfanya kukwama kwa miradi mingi katika Halmashauri hiyo.

alitoa wito kwa wananchi kuwa na imani na serikali walioichagua kwani sasa yeye kama mbunge yupo begakwabegakuakikisha anakomesha ufisadi ndani ya wilaya hiyo
Posted by MROKI On Tuesday, August 23, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo