Nafasi Ya Matangazo

July 30, 2016

 Windhoek Draught Miss Sinza 2016, Sia Pius (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na mshindi wa pili Catherine Listoni (kushoto) na mshindi wa tatu Hafsa Mahamood baada ya kutangazwa mshindi Hoteli ya Defrance lilikofanyika shindano hilo jana usiku kwa udhamini wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Ltd kupitia kinywaji wa Windhoek.
 Baadhi ya washiriki ambao hawakufanikiwa kuingia tano bora.
 Warembo walioingia tano bora. Kutoka kulia ni Catherine Listone, Sia Pius, Hafsa Mahamood, Saida Khalifa na Faith Msuya. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
 Mwakilishi wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Ltd akisema chochote kwenye shindano hilo.
 Mtoa huduma wa kampuni hiyo akitoa huduma kwa wadau wa windhoek.
 Wadau wa Windhoek ndani ya Defrance Hotel katika shindano hilo.
 Hapa ni windhoek tu kwa kwenda mbele.
 Wadau wa windhoek wakiwa kwenye shindano hilo.




 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Ltd, Jerome Rugemalira (kushoto), akigongesha chupa ya windhoek na mdau wa kinywaji hicho, iliyokatika muonekano mpya katika shindano hilo.
 Wacheza shoo wa Bendi ya Muziki wa Dansi ya FM Academia wakishambulia jukwaa katika shindano hilo.
 Wasanii wa kampuni ya mabibo wakionesha umahiri wa kucheza wakati wa shindano hilo.
 Washiriki wa shindano hilo wakijitambulisha kwa kucheza kabla ya kuanza kwa shindano hilo.
 Wanenguaji wa Bendi ya FM Academia wakiwa kazini.


 Washiriki wakiwa katika vazi la ubunifu.
 Majaji wa shindano hilo wakiwa kazini.
 "Jamani tuchangechange mapene tuongeze windhoek meza imekauka hapa"
 Hapa ni furaha tu kwa kusonga mbele.
 Majaji wakiwa tayari kuwatangaza washindi.
 Mdau wa Windhoek na mashindano ya Miss Tanzania, Rutha Lucas akitoa sh.100,000 kwa kila mshiriki wa shindano hilo ikiwa ni kifuta jasho.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Mabibo Beer Wine and Spirits Ltd, Benedicta Rugemalira (kushoto),  akimkabidhi mshindi wa kwanza wa shindano hilo kitita cha sh.500,000.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Mabibo Beer Wine and Spirits Ltd, Benedicta Rugemalira (kushoto), akimkabishi mshindi huyo moja ya katoni ya windhoek kati ya tano zilizotolewa na kampuni hiyo kwa mshindi huyo ambapo pia mshindi wa pili na watatu walikabidhiwa.

Na Dotto Mwaibale

KAMATI ya maandalizi ya shindano la Miss Sinza 2016 imemtangaza Sia Pius kuwa mshindi wa Windhoek Draught Miss Sinza 2016 baada ya kuibuka mshindi katika shindano lililofanyika Hoteli ya Defrance iliyopo Sinza jijini Dar es Salaam jana usiku.

Pius aliibuka mshindi baada ya kuwabwaga washiriki wenzake tisa waliokuwa wakiwania taji hilo ambapo nafasi ya pili ilichukuliwa na Catherine Listoni huku ya tatu ikichukuliwa na Hafsa Mahamood.

Shindano hilo lilidhaminiwa na Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spiritis kupitia bia ya Windhoek pamoja na wadhamini wengine.

Mshindi wa kwanza wa shindano hilo alizawadiwa sh.500,000 wakati wa pili akijipatia sh.300,000 na watatu akiondoka na kitita cha sh.200,000 huku washiriki wengine wakiondoka na kifuta jasho cha sh.100,000 kila mmoja.

Washindi hao watatu wataingia moja kwa moja katika shindano la kumsaka Miss Kinondoni 2016 litakalofanyika mwezi ujao.
Posted by MROKI On Saturday, July 30, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo