Nafasi Ya Matangazo

June 30, 2016

 Mkurugenzi wa Mazingira wa SABMiller Africa,Muzi Chonko akifafanua jambo katika mahojiano maalum na waandishi wa habari.
 Mkurugenzi wa Mazingira wa SABMiller Africa,Muzi Chonko akizungumza na Mwandishi wa Habari Yvonne Msemembo jijini Dar es Salaam
************
KAMPUNI ya kimataifa ya SABMiller inayomiliki viwanda vya kutengeneza vinywaji sehemu mbalimbali duniani itaendelea kufanya biashara zenye mwelekeo wa kubadilisha maisha ya jamii mbalimbali kuwa bora bila kusahau kuzingatia utunzaji wa mazingira.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Mazingira wa kampuni hiyo kanda ya Afrika Bw.Muzi Chonco,alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam ambapo alipata wasaa wa kuelezea kanuni zinazoongoza utendaji wa kazi wa kampuni kwa ajili ya kuleta mabadiliko endelevu sehemu zote ilikowekeza duniani.

Chonco alisema kuwa tangu kampuni ianze kutumia kanuni hizo ambazo zinashahabiana na malengo ya umoja wa mataifa tayari mafanikio mbalimbali yameanza kupatikana na yapo matumaini ya kufikia mafanikio makubwa katika siku za usoni.

“Tunapoongelea biashara  endelevu tunamaanisha kuwawezesha wanachi kiuchumi kama ambavyo tumekuwa tukifanya kazi na wakulima kupitia mpango wetu wa Go Farming,kuwakwamua wanawake kiuchumi,kuendeleza wajasiriamali,kutunza vyanzo va maji na kuwekeza katika miradi ya maji bila kusahau utunzaji wa mazingira”.Alisema Chonco. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.
Alitoa mfano wa kampuni  ya TBL Group ambayo iko chini ya kampuni hiyo kwa jinsi ilivyoweza kufanya uwekezaji ambao umeleta mabadiliko nchini ambapo serikali na taaasisi mbalimbali zinatambua mchango wake kwa kuitunukia tuzo mbalimbali ambazo imekuwa ikishinda mwaka hadi mwaka.

Chonco alizichambua kanuni zinazoongoza kampuni na kuleta mabadiliko kwenye jamii kuwa ni dunia yenye nuru njema,dunia changamfu,dunia imara,dunia iliyo  safi na dunia yenye nguvu kazi.

Alisema wakati umefika kwa wawekezaji mbalimbali kufanya uwekezaji wenye kuleta mabadiliko kwenye jamii badala ya kunufaisha upande mmoja “uwekezaji unaoleta ajira za kila aina kwa wananchi,unaowawezesha kujipatia mapato kwa kuuza bidhaa kwa kampuni iliyowekeza,kutunza mazingira na kuwapatia wananchi elimu ya utunzaji wa mazingira na vyanzo vva maji,kusaidia makundi mbalimbali kwenye jamii yaliyoachwa nyuma ukizingatiwa kwa vyovyote utaleta mabadiliko”.Alisisitiza.


Alitoa mfano kuwa ukimwezesha mkulima ataweza kupata kipato na kujenga nyumba nzuri ya kuishi,watoto wake kusoma vizuri,familia yake kupata lishe bora na kuongeza pato la familia kwa ujumla na maisha kubadilika kutoka hali duni kuwa bora kama ambavyo imetokea kwa wakulima na makundi mengine yanayoshirikiana na kampuni hiyo sehemu mbalimbali duniani.
Posted by MROKI On Thursday, June 30, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo