Nafasi Ya Matangazo

June 01, 2016



MIRADI ya maendeleo yenye thamani ya Sh Bilioni 1.09 inataraji kukaguliwa, kuwekewa mawe ya msingi na kuzinduliwa na Mwenge wa Uhuru Wilayani Newala mkoani Mtwara.

Mwenge huo unataraji kukimbizwa Wilayani humo kuanzia Juni 3 mwaka huu ambapo miradi nane itafikiwa na Mwenge huo utakao kimbizwa katika maeneo mbalimbali.

Akizungumza na Habarileo, Mkuu wa Wilaya ya Newala, Christopher Magala alisema miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa kituo cha afya Mkunya, uzinduzi wa Barabara ya lami Newala mjini, kuweka mawe ujenzi wa nyumba sita za walimu na kufungua kituo cha kilimo Mtangalanga.

“Mwenge wa uhuru utaanza mbio zake Wilayani Newala kuanzia Juni 3 mwaka huu na utatuzindulia miradi nane ya maendeleo ikiwa ni pamoja na kituo cha afya, nyumba za walimu, kilimo, na kutembelea vikindi vya uzalishaji mali vya vijana na wanawake,”alisema Magala.

Magala alisema Mwenge huo pia utapata fursa ya kutembelea na kujionea vikundi vya uzalishaji mali vya wanawake bana vijana ambao waliokopeshwa fedha na Halmashauri.

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya, alisema kuwa miradi hiyo nane imegharimu kiasi cha Sh bilioni 1,098629,225 ambapo kati ya hizo kiasi cha sh milioni 7,850,000 ni mchango wa jamii, huku Halmashauri ikichangia sh milioni 108,500,000 na serikali kuu ikichangia sh milioni 975,629,225.

Magala aliwaasa wananchi kujitokeza kwa wingi katika maeneo mbalimbali yatakayokimbizwa Mwenge huo ambao unakimbizwa na George Mbijima ukibeba kauli mbiu ya ‘Vijana ni Nguvu kazi ya Tifa, washirikishwe na kuwezeshwa.
Posted by MROKI On Wednesday, June 01, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo