Nafasi Ya Matangazo

June 05, 2016

Habari za J2 Wadau, pokeeni codes
Meneja Mahusiano Mwandamizi wa Benki ya Posta Tanzania Noves Moses(katikati) akionyesha fedha kissing cha shilingi milioni 8 zilizotolewa na Benki hiyo kwa ajili ya kuwasaidia vijana waendesha bodaboda wa  Wilaya ya Biharamulo. Wa kwanza kushoto Ni Mbunge wa jimbo la biharamulo Oscar Mukasa, Mkuu wa Wilaya ya Biharamulo Darry Rwegasira na kulia Ni Diwani wa kata ya Biharamulo mjini David Mwenenkundwa na Meneja wa TPB tawi la Bukoba Juvestina Tarimo.
Meneja Mahusiano wa Benki ya Posta Noves Moses (kulia) akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Biharamulo Bi.Darry Rwegasira kiasi cha shilingi milioni 8, ikiwa ni msaada wa benki hiyo kwa vijana waendesha bodaboda wa wilaya hiyo. Kushoto ni mbunge wa jimbo la Biharamulo Mh. Oscar Mukasa. Hafla ya kukabidhi msaada huo ilifanyika wilayani hapo mwishoni mwa wiki
Na Angela Sebastian, Biharamulo.
WAENDESHA pikipiki zinazofanya biashara ya kubeba  abiria katika Wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera wameshauriwa kujiunga katika vikundi rasmi na vya uzalishaji mali ili waweze kunufaika na fursa za huduma za kibanki ambazo hutolewa na banki ya posta Tanzani . BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.


Ushauri huo ilitolewa jana na mkuu wa Wilaya hiyo Darry Rwegasila wakati akifungua mafunzo ya waendesha pikipiki zaidi ya 100 waliopata mafunzo ya udereva na kupewa leseni kwa udhamini wa banki ya posta  hiyo.

Rwegasila alsema kuwa umoja ni nguvu kwahiyo wakiunda umoja wanakuwa na sauti moja pia hata viongozi  wataweza kupata mawazo yao kwa urahisi  kupiti umoja huo ili kuwatafutia fursa mbambali au kutatua changamoto zao zinazowakabili na kupandisha uchumi wao wa kipatao.

Alisema kuwa makondi hayo yatasaidia kuingia katika mfumo rasmi ambao utawawezesha kupata huduma zinazotolewa na taasisi mbalimbali kama vile banki ya posta ambazo zinalenga kuwakwamua vijana katika lindi la uamskini unaowakabili pia unaonekana kuwa  kero kubwa katika maisha yao ya kila siku.

“Mkitaka kuingia katika soko hulia lazima muwe na umoja ili muweze kufikia raslimalia zinazopatikana kama vile kupata misaada,mikopo na mafunzo kama haya waliowaletea watu wa banki ya posta kutokan ana faida wanayoipata na kugawana na wahitaji” alisema Dc.

Pia aliwashauri kuacha kufanya matumizi yasiyo ya maana ,bali watumie kidogo wanachokipata kujiwekea akiba banki ili waweze kukuza mitaji yao kwani wao ni vijana bado wanamahitaji mengi.
Kwa upande wa meneja mahusiano mwandamizi wa banki ya posta Tanzania Noves Moses alisema kuwa banki hiyo inajali wananchi ,pia vijana ni kundi kubwa lenye mchango mkubwa katika suala zima la uchangiaji wa uchumi wa Taifa.

Alisema banki hiyo walipata maombi toka kwa mbunge wa jimbo la Biharamulo Oscara Mukasa akiomba kuwawezesha vijana hao kupata mafunzo na kupewa leseni ili kuondoka ana adha ya kukimbizana na polisi kila kukicha na kupoteza muda mwisngi ambapo hushindwa kujiingizia kipatao.

Alisema banki hiyo ilikubali ombi hilo ambapo ametoa kiasi cha shilingi milioni 8 kwa ajili ya mafunzo hayo ya kupata leseniya uendeshaji wa vyombo hivyo vya moto  kwa vijana 100 kwa Wilaya ya  hiyo.

Alisema kuwa banki hiyo imejiwekea mikakati mikubwa ya kuleta na kuimalisha ustawi wa ndani ya jamii ambapo misaada mingi wanayoitoa huelekezwa katika eneo hilo ambayo hulenga masuala ya afya na elimu.

Naye mbunge wa jimbo la Biharamulo aliyeomba msada huo kwa ajili ya vijana wake Oscar Mukasa alisema kuwa ni wajibu wake kuboresha maisha ya vijana waliko jimboni mwake ili waondokane na mambo yanayoweza kuwapelekea kujiingiza katika vitendo viovu ikiwemo uvunjifu wa amani na maandamano yasiyofaa.

Mukasa alisema lengo la kuomba banki hiyo itoe msaada huo ni kuhakikisha vijana wanaepukana na maisha ya misukosuko ya kukosa leseni ambayo walikuwa wakikumba na nayo.

Posted by MROKI On Sunday, June 05, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo