Nafasi Ya Matangazo

May 24, 2016

SIKU  chache baada ya pazia  la ligi kuu ya soka Tanzania  bara kufungwa,Kocha mkuu wa Mbeya  City Fc  Kinnah Phiri ameanza zoezi maalumu la kusaka nyota wapya ambao atawajumuisha  moja kwa moja kwenye vikosi vya timu yake  msimu ujao.

Akizungumza muda mfupi baada ya majaribio ya siku ya kwanza  kwa wachezaji wapya vijana waliofika kujaribu bahati zao kwa kuonyesha  vipaji walivyonavyo navyo, afisa habari wa City Dismas Ten amesema kuwa muitikio umekuwa mzuri katika siku hii kwanza ambayo nyota hao wa baadae wamefika kuonysha  uwezo wao mbele ya kocha huyo raia wa malawi.


“Leo ni siku ya kwanza, kitu kizuri mwitikio umekuwa mkubwa, takribani vijana 50 wamejitokeza kujaribu  bahati zao kulingana na vipaji walivyonavyo, haya ni majaribio ambayo kocha Phiri ameyaitisha ili kusaka vipaji vipya ambavyo moja kwa moja vitaingia kwenye timu yetu kubwa na ile ya U20, alisema.
Posted by MROKI On Tuesday, May 24, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo