Nafasi Ya Matangazo

May 26, 2016

ZOEZI kusaka nyota wapya (vijana) ambao wataingizwa kwenye timu  mbili za Mbeya City Fc U20 na ile ya wakubwa limefikia kwenye hatua nzuri hivi sasa baada ya wachezaji 44 kupatikana kwenye mchujo wa awali  uliolifanyika  leo ikiwa ni baada ya  siku nne   za mazoezi.

Akizungumza na mbeyacityfc.com, mara baada ya kumalizika kwa mazoezi ya leo (Clinic day 5) kwenye uwanja wa Sokoine kocha msaidizi wa City, Mohamed Kijuso amesema kuwa Vijana 44 wamefanikiwa kuvuka  kwenye mchujo wa kwanza  hivyo wataingia kwenye wamu ya pili inayotaraji kuanza hapo kesho kwenye uwanja wa Sokoine.

“Tulikuwa na kundi kubwa la wachezaji zaidi ya 106, baada ya mchujo leo, tumefanikiwa kupata  44 ambao wataingia kwenye awamu ya pili hapo kesho,  lengo letu ni kuona tunapata Cream nzuri kwa ajili ya timu yetu ya vijana na pia  wachezaji saba ambao watakuwa tayari kucheza kwenye timu kubwa msimu ujao”, alisema.

Kuhusu lini itakuwa siku ya mwisho, kocha huyo kijana alitanabaisha kuwa, mchakato huu wa kuska vipaji ulikuwa ufikie tamati hapo kesho lakini uongozi wa City umeamua kusogeza mbele mpaka siku ya jumamosi  ambapo wachezaji watakaopatikana kwenye mchujo wa kesho  watapata nafasi ya kucheza mchezo mmoja wa  kirafiki na timu ya  Ilemi Fc.


“Ilikuwa tuhitimishe kesho lakini tumesogeza mpaka jumamosi ambapo vijana wetu wapya watakaopatikana watacheza mchezo wa kirafiki , na baada ya hapo zoezi litafungwa tayari wa kusubiri maandalizi ya msimu mapema mwezi ujao” alimaliza.
Posted by MROKI On Thursday, May 26, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo