Nafasi Ya Matangazo

April 20, 2016

Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha Lengay Ole Sabaya akitoa tamko kwa waandishi wa habari jana jijini Arusha,ambapo amemtaja Mathias Manga na washirika wake kuwa ni tatizo kubwa ndani ya chama na kwamba kama akiendelea kuwepo ni Dhahiri kuwa anaweza kukisambaratisha chama hicho kutokana na kugawa makundi kwa vijana wa chama hicho kutokana na fedha zake.(Habari Picha na Pamela Mollel wa jamiiblog)
Katibu Hamasa  Mkoa wa Arusha  Lucas Msomi akisisitiza jambo katika kikao na waandishi wa habari.
******************
Baraza la vijana mkoa wa Arusha la chama cha mapinduzi  uvccm limetangaza kumvua ukamanda wa vijana wilaya ya Arumeru bw,Mathias Manga kutokana na kukiujumu chama kwa muda mrefu hali ambayo imekuwa ikididimiza jitihada za kurejesha imani ya chama hicho.

 Bw,Manga ambaye ni mafanyabiashara maarufu wa madini Mkoani Arusha amekuwa akituhumiwa kwa muda mrefu kuwa namhausiano ya karibu ya aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Ukawa Edward Lowassa na kusahau kufanya majukumu ya kichama ambayo yamempa uongozi wa Ukamanda wa vijana wilaya.

 Akitoa maelezo ya tamko hilo mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha Lengay Ole Sabaya amemtaja Mathias Manga na washirika wake kuwa ni tatizo kubwa ndani ya chama na kwamba kama akiendelea kuwepo ni Dhahiri kuwa anaweza kukisambaratisha chama hicho kutokana na kugawa makundi kwa vijana wa chama hicho kutokana na fedha zake.

Aliongeza kuwa kutokana na kumvua ukamanda kamanda huyo UVCCM Mkoani hapa haitakuwa tayari kushiriki kikao chochote cha kamati ya siasa ambapo Manga atashiriki kama mjumbe katika kikao hicho.

"Sitashiriki kwa namna yeyote na vijana wangu kwenye kikao cha kamati ya siasa Mkoa ama kikao kingine ambacho kitanikutanisha na Mathias Manga na nawataka wanachama wa chama cha mapinduzi kuona kama ni halali kwa huyu aliyeitwa kamanda wa vijana kuendelea kushikilia kadi yao,"alisema Ole Sabaya

Akitoa onyo kwa makamanda wilaya ya Arusha mjini,Longido na Monduli kujipima na kujitathimini kabla ya kufikia uamuzi kama bado wanafaa kuendelea na hadhi ya ukamanda wa wilaya ama laa,na wakijiona hawatoshi tunawashauri wakae pembeni mapema kabla ya kutumbuliwa jipu.

Baraza linakiomba chama cha Mapinduzi kupitia tathini ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana wale wote walioshiriki kukihujumu chama kuanzia ngazi ya matawi,kata,wilaya na Mkoa washughulikiwe kwa mujibu wa taratibu za kimaadili kabla ya uchaguzi wa chama 2017 vinginevyo wakiachwa watashiriki tena kufanya uhasi dhidi ya chama sanjari na kupandikiza mamluki.


Hata hivyo mwenyekiti huyo ametengua uteuzi wa wajumbe watano wa baraza katika nafasi za kuteuliwa ilidumu toka mwaka 2012 na kuunda kamati mpya chini ya mwenyekiti Lengai Ole Sabaya  huku akiwataka viongozi wa chama hicho kumuunga mkono Rais JohnPombe Magufuli kwa jitihada zake za kupeperusha bendera ya chama na kufanya kazi kwa uadilifu na kubeba kauli ya HAPA KAZI TU.
Posted by MROKI On Wednesday, April 20, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo