Nafasi Ya Matangazo

April 17, 2016

Mgakuzi wa Vyakula kutoka Mamlaka a Chakula na Dawa, Dk Itikija Mwanga (kushoto) akitoa maelezo kwa Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu walipotembelea machinjio hayo, Vingunguti jijini Dar es Salaam leo. 

WIKI moja baada ya Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kuyafunga machinjio ya Ng’ombe na Mbuzi Vingunguti jijini Dar es Salaam kwa uchafu na kusababisha bei ya nyama kupanda, serikali imeitaka Halmashauri ya Manipaa ya Ilala kufanya marekebisho ya haraka ili uchinjaji uanze mara moja.
 Kaimu Mkuu wa Idara ya Mifugo katika Manispaa ya Ilala, Msongo Songoro (kulia)  akitoa ufafanuzi juu ya marekebisho yaliyoanza kufanyika machinioni hapo wakati Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu walipotembelea. 
 Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba akizungumza jambo. Kushoto ni Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala na Diwani wa Vingunguti, Omary Kumbilamoto. 
 Moja ya vitu vilivyo sababisha machinjio hayo kufungwa ni pamoja na mabomba yote ya karo za kusafishia utombo na nyama kukosa maji. Hii ilieklezwa na wasimamizi kuwa kila zinapowekwa koki huibiwa. 
 
 Mbunge wa jimbo la Segerea Bona Kaluwa akipita katika moja ya maeneo ya machinjio hayo ambayo ni machafu na nyama huuzwa humo na kuhatarisha afya za walaji. Aidha Mbunge huyo alisema kuwa kuna vitendo vichafu hufanyika machinjioni hapo nyakati za usiku. 
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (wapili kulia) akizungumza na Mkaguzi wa Chakula kutoka Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Dk Itikija Mwanga (kulia) wakati yeye na Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba (hayupo pichani) walipotembelea Machinjio ya Vingunguti Dar es Salaam jana. Kushoto ni Naibu Meya wa Ilala na Diwani wa Vingunti, Omary Kumbilamoto na wapili kulia ni Mbunge wa Segerea, Bona Kaluwa
 mawaziri hao wakiendelea na ziara yao ya kukagua mazingira ya machinjio hayo. 
 Hapa ni sehemu ya kuhifadhia nyama na kuuzwa ambayo nayo imelalamikiwa kuwa vyuma vyake vuina kutu na pia ni makosa kuuza nyama katika machinjio. 
 Kutu ilivyo katika vyuma hivyo. 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu na  Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba wakijadiliana jambo. 
Posted by MROKI On Sunday, April 17, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo