Nafasi Ya Matangazo

April 11, 2016

Mkulima wa Shahiri katika kijiji cha Nangwa wilayani Babati Peter Nade akiwa amesimama kando ya trekta lake analotumia kumrahisishia kazi zake za kilimo.
Wajumbe wa  Kamati ya Bunge ya Biashara,Viwanda na Mazingira wakiwa kwenye mashamba ya wakulima wa Shahiri wilayani Monduli katika ziara waliyoifanya hivi karibuni.
Wajumbe wa  Kamati ya Bunge ya Biashara,Viwanda na Mazingira wakiwa kwenye mashamba ya wakulima wa Shahiri wilayani Monduli katika ziara waliyoifanya hivi karibuni.
HAKUNA ubishi kuwa kilimo ni uti wa mgongo wa wananchi wengi wanaoishi barani Afrika pia kilimo ni njia pekee ya kuwawezesha wananchi wengi kwenye jamii za Kiafrika kujikwamua kiuchumi na kuwezesha nchi nyingi kupiga hatua kwa kuinuka kiuchumi pia sekta hii inayo nafasi kubwa ya kupunguza tatizo la ajira ambalo limekithiri hususani kwa vijana.

Pamoja na fursa zilizopo kwenye sekta ya kilimo bado wakulima wengi barani Afrika ni maskini wa kutupwa na wanakabiliwa na changamoto nyingi zinazowafanya waishi maisha duni ya kushindwa kikidhi mahitaji yao na wengi wao mazao wanaozalisha hayawatoshelezi pia kwa mahitaji yao ya chakula.Majanga ya kulia njaa kwenye nchi nyingi za Kiafrika ni jambo la kawaida.

Wakati tatizo la kukomboa maisha ya wakulima wadogo kimaisha kuendelea kuwa kitendawili kisicho na jibu miaka miaka hadi miaka,nuru imeanza kuonekana kutokana na kufunguliwa kwa milango ya uwekezaji wa aina mbalimbali ambapo kuna baadhi ya makampuni yamewekeza barani Afrika ambayo tayari yameonyesha kuwa na dhamira ya kufanya kazi na wakulima wadogowadogo wanaozalisha malighafi kwa viwanda vinavyomilikiwa na makampuni hayo badala ya kukamata ardhi na kuingia kwenye sekta ya kilimo yenyewe.

Moja ya kampuni ambayo imewekeza barani Afrika na imeanza kufanya kazi na wakulima wadogowadogo kwenye nchi mbalimbali na ikiwa na mpango wa kupanua wigo wa kusaidia wakulima wadogo ili waweze kuwa na uzalishaji wenye tija na kuiuzia mazao ni SABMiller ambayo imefanya uwekezaji katika viwanda vinavyotengeneza vinywaji. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.
Katika Baadhi ya nchi ambapo imeanza kufanya kazi na wakulima wadogo ikiwemo Tanzania  ambapo tayari imeanza kufanya kazi na wakulima wa zao la Shayiri katika mikoa ya Kaskazini ya Arusha na Kilimanjaro tayari wakulima wameanza kuonja matunda ya ushirikiano huu kwa kuwa wanawezeshwa kuendesha kilimo cha kisasa,kupatiwa pembejeo,mbegu na wataalamu wa kutoa ushauri na wanakuwa na soko la uhakika kwa ajili ya kuuza mazao yao.

Peter Nade ,mmoja wa wakulima wa zao la Shayiri wilayani Babati Mkoani Arusha na baba mwenye watoto sita anatoa ushuhuda wa maisha yake yalivyokuwa hapo awali kabla hajaanza kilimo cha zao la Shayiri“katika miaka ya nyuma nilikuwa mkulima wa zao la mahindi katika kipande kidogo cha ardhi na maisha yalikuwa magumu kutokana na udogo wa kipato na kutopata chakula cha kutosheleza mahitaji ya familia yangu.Tangu nianze kilimo cha zao la Shayiri nikiwa kwenye kikundi kinachoshirikiana na kampuni ya TBL Group  maisha yangu yamebadilika na kuwa bora “.

Nade anaendelea kuelezea kuwa hivi sasa anamiliki shamba la ekari 200 na anafanya kilimo cha kisasa  akiwa na nyenzo za kisasa za kilimo na anawezeshwa kuendesha kilimo cha Shayiri kwa kujiamini kwa msaada anaopata kutoka kampuni ya Tanzania Breweries Limited.

Jambo la kufurahisha analolielezea Nade  ni kuwa maisha yake yamebadilika kuwa bora ambapo  kwa sasa anamudu kuwasomesha watoto wake katika shule nzuri wilayani Babati na anamiliki trekta linalomsaidia kurahisisha kazi  yake ya kilimo.

Mkulima mwingine wa Shayiri wa Monduli Nainoto Maliaki ambaye ni mjane amesema anamudu maisha na kusomesha watoto wake na ameweza kujenga nyumba ya kisasa.Kwa  upande wake Onesmo Kway naye mkulima wa shayiri na yuko kwenye kikundi kinachoshirikiana na TBL anasema kilimo cha Shayiri kimebadilisha kabisa maisha yake ambapo kimemuwezesha kujenga nyumba nzuri na anawasomesha watoto wake bila matatizo.

Shuhuda wa mafanikio na zinazotia matumaini haziko kwa wakulima wa Shayiri wa Tanzania peke yake bali ni kutoka nchi mbalimbali barani  Afrika ambako kampuni ya SABMiller imefanya uwekezaji na kuazisha mpango unaojulikana kama Go Farming wa kushirikiana na wakulima wadogowadogo kwa kuwawezesha na kununua mazao yao ambayo ni malighafi ya kutengenezea vinywaji vinavyozalishwa kwenye viwanda vyake.

Lengo kubwa la mpango huu ni kuinua maisha ya wakulima wadogowadogo,kuongeza kasi ya kukua uchumi na kujenga mfumo mzuri na endelevu wa  kupata malighafi kwa ajili ya viwanda vyake vilivyopo kwenye nchi mbalimbali barani Afrika

Mpango wa Go Farming haulengi kunufaisha wakulima wa Shayiri pekee bali pia wa mazao mengine kama mtama na mihogo na katika siku za usoni wakulima wa zao la mahindi watawezeshwa pia na inategemewa hadi kufikia mwaka 2020 zaidi ya wakulima nusu milioni watakuwa wamewezeshwa sehemu mbalimbali duniani ambako kampuni imewekeza.

Matarajio ya mafanikio ya mpango huu katika kipindi cha mwaka 2015 hadi 2020 yanaonyesha kukua kwa asilimia 44 katika nchi 10 ambako umeanza kutekelezwa na inakadiriwa kuwepo ongezeko la uzalishaji wa mazao kutoka tani 300,000 kufikia zaidi ya tani 600,000.

Mpango huu wa kampuni kutegemea kupata malighafi kutoka  hapa nchini umeungwa mkono na serikali za nchi mbalimbali ikiwemo Tanzania kwa kuwa unalenga kuinua hali za maisha za wananchi hasa wakulima ambao wana hali duni,hali hii imepelekea baadhi ya nchi kuipunguzia kodi ya zuio kampuni inapofanya uzalishaji kwa malighafi zilizonunuliwa ndani ya nchi .

Hivi karibuni Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira ilipata fursa ya kutembelea wakulima wa zao la Shayiri wanaoshirkiana na TBL Group na baadhi ya wajumbe wa kamati hii walipongeza mpango huu wa kushirikiana na wakulima kuwa utaweza kuinua sekta ya kilimo nchini kwa haraka na kuboresha maisha ya wakulima.


Huu ni mfano wa uwekezaji wenye faida kwa watanzania kwa kuwa unaeleta mabadiliko kwenye jamii na kubadilisha maisha ya wananchi wengi kuwa bora.
Posted by MROKI On Monday, April 11, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo