Nafasi Ya Matangazo

November 05, 2015


Wapenzi wa muziki nchini ambao wanafuatilia onyesho la Coke Studio kupitia luninga ya Clouds ambalo limeanza kuonyeshwa hivi karibuni wamesema linaleta burudani na Kolabo(mash-up) za mwaka huu imeshirikisha wanamuziki wenye mvuto na kipaji kikubwa.

Wakitoa maoni yao baada ya show ya nguli wa Bongleva Fid Q kutoka nchini na Maurice Kirya kutoka nchini Uganda walisema onyesho hili mwaka huu limezidi kuwa bora na kuleta raha kwa wapenzi wa muziki.

Walisema kuwa show hizi zimerekodiwa kwa viwango vya juu  vinavyokubalika  kimataifa mbali na kushirikisha wanamuziki wazuri wenye mvuto mkubwa katika anga ya muziki.

Jane Saimon Mwanafunzi wa Chuo cha IFM kilichopo Dar es salaam anasema “Napenda sana Mash up ya Coke Studio iko bomba na imeshirikisha wanamuziki wazuri.

Mkazi wa Mwanza Aliyejitambulisha kwa jina la Dj.Pancras alisema kolabo (Mash up) za coke Studio mwaka huu zinavutia kiasi kwamba yeye na wenzake siku ya  onyesho hilo hawabanduki kwenye luninga.

Ally Katola wa Arusha alisema “Coke Studio ni bomba kiasi kwamba mimi na wenzangu hatukosi kamwe omnyesho hili ambalo lina wanamuziki nguli kutoka nchini na nchi nyingine za Afrika”.

Suzana Mwakyoma wa Mbeya anasema “Nampenda Vanessa na Ali Kiba na kuwa kwao kwenye Coke studio kunalifanya onyesho hili liwe na mvuto mkubwa”.

Mustafa Abdul mkazi wa Tanga anasema Coke Studio ni kisima cha burudani na ni onyesho mojawapo la muziki lenye mvuto wa pekee  kupitia kwenye luninga.

John Peter mkazi wa Moshi anasema “Nimekuwa mpenzi wa onyesho la Coke studio tangia lilipoanzishwa  na linaleta burudani kwa  wapenzi wa muziki vijana kwa wazee.

Wasanii wanne kutoka Tanzania waliopo kwenye show ya Coke Studio mwaka huu   ni Ben Pol ambaye anafanya mash up pamoja na  mwanamuziki nguli kutoka Kenya anayejulikana kama Wangechi, Fid Q anafanya mash up na Maurice Kirya kutoka Uganda, Gwiji wa Bongo fleva nchini Ali Kiba anafanya mash up  na Victoria Kimani kutoka nchini Kenya na wakati Vanessa Mdee anafanya mash up na  mwanamuziki nguli kutoka nchini Nigeria ajulikanaye kama 2Face.
Posted by MROKI On Thursday, November 05, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo