Nafasi Ya Matangazo

August 01, 2015

Mpendwa Mama Rhoda Cleopa Msuya Daima tutakupenda kamwe hatutokusahau. Ni Miaka kumi tangu ulipotangulia tumebaki na kumbukumbu za mapenzi yako ya dhati na wema wako Tumekukumbuka leo, jana, juzi na siku kabla yake Tunakukumbuka moyoni na kila tunapotaja jina lako. 
 
Kumbukumbu zetu kwako haziwezi kuelezeka tumebaki na kumbukumbu ya tabasamu lako na picha yako Ni kumbukumbu za upendo wako ndio zinatupa nguvu ya kuendelea mbele Daima utabaki katika mioyo yetu Uko Katika Ufalme wa Mungu, Tunakuombea upumzike kwa amani.

Unakumbukwa daima na mume wako Cleopa, watoto wako George,John,Joyce, Job, Naanjela. Wakwe, Onesmo, Khadija,Mercy,Mary na Yoko, wajukuu, ndugu na marafiki.

Misa maalum ya kumbukumbu ya wapendwa wetu Mama Rhoda Cleopa Msuya na Geoffrey Cleopa Msuya itafanyika Tarehe 9 August 2015 kwenye kanisa la Azania Front Cathedral saa tatu na nusu asubuhi,
Wote mnakaribishwa.

“kuwakumbuka wenye haki huwa na baraka” Mithali 10:7
Posted by MROKI On Saturday, August 01, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo