Charles Mihayo has been jailed for life for murdering his two young daughters.
Charles Amon Mihayo (36) Mtanzania mwemye makazi ya kudumu anayeishi mjini Melbourne, nchini Austaralia,   amehukumiwa kifungo cha maisha jela baada ya kutiwa hatiani katika kesi ya mauaji iliyokuwa ikimkabili.
Mihayo alikuwa akikabiliwa na kesi ya mauaji ya kikatili dhidi ya watoto wake wawili kosa alilolitenda ili kulipiza kisasi kwa mkewe baada ya kumuacha.
Mihayo alifanya ukatili huo kwa wanae Savannah (4) na Indianna (3) Aprili 20, 2014 nyumbani kwake huko Melbourne wakati wakicheza mchezo wa kujificha na kutafuta vitu wakati wa sherehe ya Pasaka, amehukumiwa leo kifungo hicho.
Inadaiwa kuwa baada ya kuachwa na mke wake, hasira zilimfanya bwana Mihayo kuamua kufanya ukatili wa kukatisha uhai wa watoto wake mwenyewe Savannah (4) na Indianna (3), ili tu kumuumiza mke wake kama njia ya kumlipizia kisasi. Inadaiwa kuwa aliwauwa kwa kuwakandamiza na mto baada ya kucheza nao.
Taarifa hiyo inaeleza kuwa siku mauaji hayo yalipofanyika, mama wa watoto hao aliwapeleka kwa baba yao bwana Mihayo, kufuatia ombi la mzazi mwezake kutaka kuwaona watoto wake hao kwa mara ya mwisho na kuwaaga.
Aidha inaelezwa kuwa Mihayo aliwanunulia nguo mpya na viatu watoto wake .
Kabla ya kutenda ukatili huo kwa damu yake mwenyewe, Mihayo aliwarekodi video wakicheza muziki huku akicheza nao. 
Baada ya kuwauwa aliwaogesha na kisha kuwavalisha nguo mpya alizo wanunua na kuwaweka vyema na kuwapigia simu Polisi.
Mtalaka wake huyo anae ishi mtaa jirani na Mihayo akiwa na mama yake walikaa jirani na mara zote walisikia watoto wakicheza lakini mara wakaona kimya kimetawala aliamua kubisha hodi mara kadhaa ndipo Mihayo akamjibu  
 "Utafahamu pindi watakapo fika hapa," na kbla ya mtalaka wake huyo kwenda kupiga simu polisi askari walifika na Mihayo kufungua mlango mkononi akiwa na taulo na kusema “Tayari, nimewaua. Nimewaua watoto wangu. Inabidi mumuulize huyu (mama yao) sababu.”.
Awali katika video ambayo polisi baadae waliiona, alisikika akiwaambia binti zake wamuoneshe mama yao nguo mpya alizowanunulia, na walifanya hivyo na kisha mwanaume huyo akakaa mbele ya camera na kusema “tutamuonesha mama kitu kingine dakika kumi zijazo”, na kuendelea kucheza nao hadi alipowakandamiza na mto (pillow) hadi kufa.
Polisi waliwakuta watoto hao wakiwa tayari wamefariki huku wakiwa wamevalishwa nguo na viatu vipya ambavyo walinunuliwa na baba yao siku hiyo.
Huku hiyo ya Jaji Lex Lasry wa Mahakam Kuu ya Victoria,  itamlazimu  Charles Mihayo kutumikia kifungo cha miaka 31 kabla ya kupata haki ya kupewa msamaha.
Savannah (4) kulia akiwa na mdogo wake Indianna (3)