Nafasi Ya Matangazo

September 28, 2014

 Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasiliamali Watu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Bw. D. Mndeme (kushoto) akizungumza na wanamichezo wa Ofisi yake wakati akiwaaga na kukabidhiwa vifaa vya michezo leo asubuhi kwa ajili ya kuelekea Mjini Morogoro kushiriki katika michuano ya Shimiwi iliyofunguliwa leo. Katikati ni Afisa Utawala wa TTCL Tanzania, Ulrick Swai (kulia) ni Katibu wa timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Bw. Mandia.

  Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasiliamali Watu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Bw. D. Mndeme (kushoto) akipokea sehemu ya vifaa vya michezo (jezi) kutoka kwa Afisa Utawala wa TTCL Tanzania, Ulrick Swai, wakati wa hafla fupi ya kuagwa timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais na kukabidhiwa vifaa vya michezo leo asubuhi kwa ajili ya kuelekea Mjini Morogoro kushiriki katika michuano ya Shimiwi iliyofunguliwa leo. Kulia ni Katibu wa timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Bw. Mandia.
 Picha ya pamoja baada ya makabidhiano hayo....
Baadhi ya wanamichezo wa Ofisi ya Makamu wa Rais, wakipanda katika basi tayari kwa safari kuelekea Morogoro.
Posted by MROKI On Sunday, September 28, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo