Nafasi Ya Matangazo

June 11, 2013

WASANII wa filamu nchini wameshauriwa kuwasilisha miswada ya filamu kwa Bodi ya Filamu ilkaguliwe na kupewa kibali kama unafaa,umefata sheria na haujakiuka maadili ya sheria ya Filamu na Michezo ya kuigiza pamoja na kanuni zake.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bi.Joyce Fissoo wakati wa kikao na mtengenezaji wa filamu Aunt Ezekiel kuhusiana na kazi yake mpya ijulikanayo kama Scola.

Katibu huyo amefafanua kuwa kuna umuhimu wa wasanii kufata sheria  na taratibu za filamu kabla ya kuanza kutengeneza na kuzitoa filamu zao ambapo sheria inawataka kuwasilisha  miswada (script) Bodi ya filamu ili ukaguliwe na kupewa idhini yakuendelea na kazi hiyo.

“Wasanii mnatakiwa kuzingatia sheria na kuwasilisha script ili zikaguliwe na kupata ruhusa kwa mujibu na taratibu za sheria kabla ya kuanza kutengeneza filamu kwa sababu sheria Na 4 ya mwaka 1976 ya Filamu na Michezo ya Kuigiza pamoja na kanuni zake zinataka wasanii kutotoa au kutengeneza filamu kabla ya kupeleka mswada(script ) kwa Bodi.

Aidha Katibu huyo amefafanua kuwa wasanii wanapotengeneza picha kupitia script ambazo hazijakaguliwa kuna uwezekano mkubwa wakuwepo sehemu ambazo zinakiuka maadili ya mtanzania,ikiwepo uvaaji wa mavazi mafupi yaliyopitiliza kwa waigizaji wanawake,lugha mbaya na baadhi ya vitendo vingine visivyofaa kuoneshwa kwa umma.

Bi Fissoo amesema kuwa Bodi imepewa mamlaka kwa mujibu wa Shetia kuzuia filamu hizo ambazo hazijakaguliwa ,na kama msanii hajafuata sheria atapata hasara kutokana na gharama ambazo atakuwa ametumia na endapo filamu hiyo itafutwa, jambo a,balo Bodi isingelipenda liwakute wadau wake.

Kwa upande wake Msanii wa Filamu za Kiswahili Aunty Ezekiel ameomba radhi kwa kutoleta script yake ya filamu hiyo mpya ya SCOLA Bodi ya Filamu na ameahidi kurekebisha baadhi ya vipengele kama alivyoelekezwa na Bodi hiyo kwani vitu hivyo vinaweza kurekebishika.

Aunty Ezekiel amefurahishwa sana na kuishurukuru Bodi ya Filamu Tanzania kwa kufanya majadiliano mazuri juu ya filamu yake kwa kubaini mapungufu yaliyopo na ameahidi kuyafanyia kazi ili kuboresha filamu hiyo na pia amewaasa wasanii wengine wote kuwa na imani na Bodi ya Filamu na kutokuwa na dhana tofauti juu ya Bodi hiyo.
Aunty Ezekiel ni msanii aliyetengeneza filamu nyingi hapa nchini ambazo zinasambazwa na Kampuni ya Steps Entertainment iliyopo hapa nchini.
Posted by MROKI On Tuesday, June 11, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo