Nafasi Ya Matangazo

May 15, 2012

Tanzania leo imeungana na nchi nyingine ulimwenguni kufanya maadhimisho ya siku ya Familia, hapa nchini watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi bila ya uangalizi wa Wazazi au walezi imekuwa ikiongezeka siku hadi siku.

Leo hii Camera ya FK Blog ilimulika watoto hawa wa Mjini Singida ambao maisha yao ni sawa na ndege, hawajui wanakula nini, wanavaa nini, kuoga au mahali pa kujilaza.

Wengi wanawaita watoto wa Mtaani, lakini ukweli ni kuwa hakuna mtoto wa mtaani, bali watoto wote wanatoka katika familia ambayo ni muungano wa Baba na Mama. Panapotokea mifarakano ya waanzilishi wa familia na kila mmoja kwenda ajuako, ndipo watoto nao huingia katika maisha ya malezi ya upande mmoja. 

Mahojiano ya kila matra yanayofanywa na vyombo vya habari na wataalam wa mambo ya Ustawi wa jamii hubaini kuwa wingi wa watoto hao mtyaani ni chimbuko la mifarakano ya wana familia wawili. 

Baba anapo mtaliki mama na kuoa mke mwingine amekuwa akileta unyanyasaji na kufanya motto kukimbia nyumbani, kadhalika pia mama akiolewa sehemu nyingine baba wa kurithi hana mapenzi na malezi bora kwa mtoto.

Jamii haina budi kubadilika na kutatua migogoro ya familia na kuzaa kabla ya wakati na kushindwa kutoa huduma bora kwa watoto wa namna hii. 

Hawa ni watoto wetu na si watoto wa mtaani, tuwalee!

Posted by MROKI On Tuesday, May 15, 2012 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo